Poems

Kifungoni

Kwa kuangulia juu mbinguni

na kulia sana kwa matumaini
samawati imeingia
                              mwangu machoni.
Kwa kuota mahindi mashambani
na kulia sana kwa mahuzuni
manjano imeingia
                              mwangu machoni.
 
Waache majemadari waende vitani
Wapenzi waende bustanini
Na waalimu mwao darasani,
            Ama mimi, tasubihi nipeni
            Na kiti cha kale, za zamani
            Niwe vivi nilivyo duniani:
                        bawabu mlangoni
                        katika kingo ya maumivu ya ndani
            maadamu vitabu, sheria na zote dini
zitanihakikishia mauti
                                    nikiwa na njaa au kifungoni.