Poems

Mlango

Ama utapita

katika mlango huu
au hutapita.
 
Ukipita
kuna hatari
ya jinalo kulisahau.
Hayo ni matata
 
Mambo hukutizama mara mbili mbili
Nawe sharuti utazame kando
uwache yatendeke.
                Usitafute vita.
 
Usipopita
Huenda ukakuta
maisha mema ya kufuata
 
ukahifadhi mawazo yako
ukaendelea na kazi yako
ukafa kishujaa nchini mwako
 
lakini mengi huenda yakakupita
mengi yakakupofua, upofu ukakupata
kwa gharama gani? Sijui.
 
Mlango wenyewe
haumuahidi mtu kitu
Ni mlango tu!